Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amempokea Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Paul Kagame ambaye amewasili nchini kushiriki Mkutano wa Pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 8 Februri, 2025.
Aidha, kwa upande wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Rais Felix Tshisekedi amemtuma Waziri Mkuu wa DRC, Judith Suminwa kumuwakilisha katika Mkutano huo.
Jumuiya zote mbili zinakutana kujadili kwa lengo la kupatia ufumbuzi hali ya ulinzi na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.